Timu ya taifa ya Kenya Harambee Star nao wakalala kwa kufungwa mabao 2-0 na Cape Verde.
Mabao ya Cape Verde yalifungwa na Heldon Ramos dakika ya 45 na dakika ya 52 na wakabanduliwa kwa jumla ya 2-1 baada yao kushinda 1-0 mechi ya mkondo wa kwanza iliyochezewa Nairobi.
Rwanda nao wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani Kigali walifungwa na Libya kwa mabao 3-1. Mounir alifungia Libya bao la kwanza dakika ya 36, la pili wakafungiwa na Mohamed Ghanudi dakika ya 48 na kisha Mounir akaongeza la tatu dakika ya mwisho.
Bao la kufutia machozi la Rwanda lilifungwa na Jacques Tusiyenge dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza.
Rwanda walibanduliwa kwa kushindwa kwa jumla ya 1-4 baada yao kulazwa 0-1 mechi ya mkondo wa kwanza ugenini.
Matokeo mengine ya mechi zilizochezwa Jumanne ni kama ifuatavyo:
Cameroon 0-0 Niger (Jumla 3-0)
Congo 2-1 Ethiopia (Jumla 6-4)
Nigeria 2-0 Swaziland (Jumla 2-0)
Ghana 2-0 Comoro (Jumla 2-0)
Misri 4-0 Chad (Jumla 4-1)
Ivory Coast 3-0 Liberia (Jumla 4-0)
Tunisia 2-1 Mauritania (Jumla 4-2)
Afrika Kusini 1-0 Angola (Jumla 4-1)
Burkina Faso 2-0 Benin (Jumla 3-2)
Senegal 3-0 Madagascar (Jumla 5-2)
Mali 2-0 Botswana (Jumla 3-2)
Chapisha Maoni